Loading...
Sheria ya Makosa Ya mtandao yanasa watano Ambao Hutengeneza Message FEKI Za Wanasiasa
![]() |
| Kamanda Kova |
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleimani Kova alisema watu hao wamekuwa wakitumia vibaya majina ya watu maarufu hasa wanasiasa.
Kova alitaja majina ya wanasiasa yanayotumiwa vibaya kuwa ni mgombea ubunge Jimbo la Kibamba, John Mnyika na mgombea urais wa Chadema chini ya mwamvuli wa Ukawa, Edward Lowassa na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.
Aliwataja watuhumiwa hao, kuwa ni Joel Lumbay (32), Omar Suleiman wote wakazi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Michael Nickson (32) mkazi wa Tegeta, Patrick Natala na Maxmillian Msacky wakazi wa jijini Dar es Salaam.
Alisema watu hao, wamekuwa wakituma ujumbe mbalimbali wakionesha viongozi hao walikuwa wanajadili jambo fulani dhidi ya kundi au chama kingine cha siasa kwa kutumia mitandao.
“Wana tabia ya kutengeneza ujumbe mfupi wa maneno (SMS) kwa lugha iliyozoeleka kama ‘kuchati,’ lakini mawasiliano hayo hayapo… yanakuwa yametengenezwa ili kutimiza malengo yao. Jambo hili ni kosa la jinai na linaweza kuchochea chuki katika makundi ya watu,” alisema Kova.
Alisema jeshi hilo linaendelea kuwasaka watu hao kwa kushirikiana na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA).
“Kiongozi au mtu yeyote atakayeona ameathirika na mbinu chafu za kihalifu asisite kutoa taarifa kwa vyombo vya dola ili hatua za kisheria zichukuliwe mara moja,” alisema.
Diamond Azidi Kukata Watu Kidomo.... Ashinda tuzo mbili za African NAFCA
Diamond Platnumz anaendelea kufanya vizuri kimataifa baada ya kuibuka mshindi wa tuzo mbili za African NAFCA.
Muimbaji huyo ameshinda vipengele vya msanii wa mwaka anayependwa pamoja wimbo wa mwaka unaopendwa ‘Nana’ aliomshirikisha Flavour.
Kupitia Instagram, Diamond ameandika:
I would love to say thank you to everybody who Voted for me on @africannafca Awards…am so grateful, i wouldn’t have Made it without you…hare are our Trophies….i will always make sure i work hard to make My Africa Proud..also wanna Thank @africannafca for keep Supporting African talents….please, don’t forget to Vote for me on @MtvEma awards.
Muimbaji huyo ameshinda vipengele vya msanii wa mwaka anayependwa pamoja wimbo wa mwaka unaopendwa ‘Nana’ aliomshirikisha Flavour.
Kupitia Instagram, Diamond ameandika:
I would love to say thank you to everybody who Voted for me on @africannafca Awards…am so grateful, i wouldn’t have Made it without you…hare are our Trophies….i will always make sure i work hard to make My Africa Proud..also wanna Thank @africannafca for keep Supporting African talents….please, don’t forget to Vote for me on @MtvEma awards.
Wafanyakazi waliofichua ukweli kuhusu kikao cha Dr. Slaa Serena Hotel wafukuzwa kazi
Katika mkutano huo alitangaza rasmi kujivua Ukatibu Mkuu wa Chadema na uanachama pia wa Chama hicho na kueleza kuwa anastaafu kabisa shughuli za siasa na kwa hiyo akaeleza kuwa hana nia ya kujiunga na chama chochote cha siasa.
Hata hivyo katika kikao hicho ambapo alitumia zaidi ya saa 1 kuongea ambapo alikitumia kikao hicho karibu chote kuporomosha mashambulizi mfululizo kwa chama chake cha Chadema na vyama vinavyounda Ukawa na kumshambulia Edward Lowassa kwa nguvu zake zote na kumuita fisadi mkubwa na kukilaumu chama chake kwa kumpokea Lowassa na kupewa fursa ya kugombea Urais kwa tiketi ya chama cha Chadema kuwa ni sawasawa na kukihamisha choo kutoka chumbani na kukipeleka sebuleni.
Baada ya kikao hicho kwisha kesho yake ikatumbukizwa clip kwenye mitandao ya kijamii ambapo mfanyakazi mmoja wa kike wa Hoteli hiyo aliyatambulika kwa jina la Neema alisikika akielezea namna kikao hicho kilivyoandaliwa na kugharimiwa gharama zote na KITENGO na namna Dr Slaa alivyokuwa amepangiwa chumba katika Hoteli hiyo na KITENGO siku moja kabla na kuwa siku hiyo kabla ya kufanyika kikao hicho Dr Slaa alilala hotelini hapo akiwa na 'mchumba' wake Josephine Mushumbusi.
Dada huyo jasiri na shujaa aliendelea kueleza kwenye clip hiyo namna watu wa KITENGO wakishirikiana na idara ya usalama wa Hoteli hiyo ambavyo walikuwa wakimuingiza kwa kificho hotelini hapo Dr Slaa na mkewe pamoja na Dr Mwakyembe ambaye alikutana na Dr Slaa na kuongea naye kwa masaa matatu kabla ya kikao chake hicho na waandishi wa habari kwa kupitia 'mlango wa nyuma' ambao kwa kawaida hutumika tu na wafanyakazi wa Hoteli hiyo.
Taarifa ambazo zimepatikana ni kuwa Mfanyakazi huyo Neema pamoja na Afisa Mkuu wa Usalama wa Hoteli hiyo pamoja na Msaidizi wake upande wa Usalama, tayari wamashafukuzwa kazi kwa 'maagizo' toka mamlaka za juu za nchi yetu.
Inasemekana pia kuwa wafanyakazi hao hawakupewa hata fursa ya kutoa utetezi wao kwa tuhuma hizo kwenye kikao cha Nidhamu kama ilivyo utaratibu wa kawaida wa Hoteli hiyo na ambavyo pia ni kinyume kabisa cha principle kuu ya Natural Justice ya right to be heard.
Hivyo basi kutokana na taarifa hizo za kutimuliwa kwa wafanyakazi hao kujulikana hivi sasa upo umuhimu mkubwa wa wakereketwa wa haki za binadamu,viongozi wanaounda muungano wa Ukawa na wananchi wengine kwa ujumla wao kulifuatilia kwa karibu suala hilo na kuhakikisha kuwa uonevu huo uliofanywa na serikali hii ya Sisiem dhidi ya wafanyakazi hao unakomeshwa na wafanyakazi hao warejeshwe kazini.







